Ikulu ya Ufaransa leo imetoa taarifa ikisema, rais Macron ameidhinisha barua ya kujiuzulu ya waziri mkuu wa nchi hiyo Edouard Philippe.
Taarifa imesema Bw. Philippe na mawaziri wote wa serikali wataendelea kufanya kazi mpaka serikali mpya iundwe.
Rais Macron amekubali na baada ya hapo amemteua Jean Castex kuwa waziri mkuu mpya.
Habari kutoka televisheni ya BFMTV zinasema, mkutano wa mawaziri uliopangwa kufanyika asubuhi ya leo umefutwa.
Habari nyingine zinasema, katika duru ya pili ya uchaguzi wa miji nchini Ufaransa, Bw. Philippe amechaguliwa meya wa mji wa Le Havre.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |