Kwa mujibu wa Idara ya posta ya China, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, sekta ya usafirishaji wa vifurushi ya China imeondoa athari ya mlipuko wa maambukizi ya virusi vya Corona na kutarajia kumaliza usafirishaji wa vifurushi bilioni 34 ambayo imeongeza kwa asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana. Mapato ya usafirishaji huo yameongezeka kwa asilimia 12 na kuzidi dola za Marekani bilioni 54.7.
Naibu mkurugenzi wa Kituo cha maendeleo na utafiti cha idara hiyo Bw. Hu Kai amesema, ongezeko hilo linatokanana na sekta hiyo kuanza mapema kazi tena na uhamiaji wa soko la mauzo kwenye mtandao wa Internet.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |