• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wanasiasa wa Marekani wahimizwa kuacha kauli na vitendo vya kuharibu uhusiano kati ya China na Marekani

    (GMT+08:00) 2020-07-29 19:26:02

    Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Wang Wenbin amesema, kauli za baadhi ya wanasiasa wa Marekani haswa waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Bw. Mike Pompeo zinazosema kwamba mawasiliano kati ya Marekani na China yameshindwa, haiheshimu historia na wala hailingani na ukweli.

    Bw. Wang amesema China inawataka wanasiasa hao wa Marekani waache mawazo ya vita baridi, kuutazama uhusiano kati ya China na Marekani kwa usahihi, na kuacha mara moja kauli na vitendo vinavyoharibu uhusiano huo, ili kuanzisha mazingira ya lazima kwa ajili ya kurejea kwa uhusiano wa kawaida kati ya nchi hizo mbili.

    Bw. Wang amesema uhusiano kati ya China na Marekani unahusisha neema, amani na utulivu duniani, na katika karibu miaka 50 iliyopita tangu nchi hizo mbili zianzishe uhusiano wa kibalozi, mawasiliano na ushirikiano kati yao vimeendelea kukua na kupanuka, na kuwanufaisha sana wananchi wao.

    Bw. Wang amesisitiza kuwa dunia ina rangi tofauti, ingawa China na Marekani zina mifumo tofauti ya kijamii, lakini zinaweza kuishi pamoja kwa amani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako