Shirika la afya duniani WHO limetangaza kuunda timu ya ushauri wa kiufundi kuhusu uchambuzi wa mienendo na sayansi za afya ikiwa ni hatua mpya ya kupambana na virusi vya Corona.
Mkurugenzi wa Who Bw. Tedors Ghebreyesus ameuambia mkutano uliofanyika kwa njia ya video, kuwa hatua hii itapanua na kuhimiza kazi ya WHO kuhusu sayansi za tabia, na kuunga mkono kazi zake katika kutoa ushauri kuhusu afya ambao sio tu ni imara zaidi, bali pia wenye ufanisi zaidi.
Kikundi hicho kitakuwa na wataalamu 22 kutoka nchi 16, wenye utaalamu kuhusu saikolojia, anthropolojia, uhimizaji wa afya, sayansi ya neva na maeneo mengine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |