Mkuu wa mkoa wa utawala maalumu wa Hong Kong Bibi Carrie Lam ametangaza kuwa uchaguzi wa bunge la mkoa huo umeahirishwa kwa mwaka mmoja. Hii ni mara ya kwanza kwa Hong Kong kuahirisha uchaguzi huo tangu irudi kwa China.
Bibi Lam amesema kwa kufuata sheria ya hali ya dharura, uchaguzi huo unaofanyika kila baada ya miaka minne umeahirishwa, ili kuhakikisha usalama wa umma na afya ya wakazi wa Hong Kong.
Uchaguzi wa bunge la awamu ya saba la Hong Kong ulipangwa kufanyika tarehe 6, Septemba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |