Mauzo ya nje ya kenya kwa nchi tatu zinazoongoza katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ilishuka katika robo ya pili hadi mwezi Juni. Hii inaonyesha athari za vikwazo vya kusafiri zilizowekwa kukomesha kuenea kwa janga la virusi vya corona.
Mapato kutoka kwa bidhaa zilizouzwa kwenda Uganda, Tanzania na Rwanda yalifikia Sh20.06 bilioni katika kipindi cha Aprili-Juni, kutoka Sh25 bilioni.
Kushuka kwa asilimia 20.2 ilirekodiwa wakati wafanyabiashara wa Kenya walishuhudia ucheleweshaji wa muda mrefu katika mpaka kwa sababu ya mahitaji ya cheti ya vipimo vya corona kwa madereva wa malori.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |