Shirika la Maendeleo laUmoja wa Afrika (AUDA-NEPAD)limezindua mpango wa kusaidia Biashara ndogo ndogo na za Kati barani Afrika kujikinga na athari mbaya wakati huu wa janga la COVID-19.
AUDA-NEPAD, kwa kushirikiana na Ecobank , zilizindua taasisi ya kutoa mafunzo na rasilimali kwa biashara hizo katika nchi mbalimbali.
Jukwaa hilo pia litatoa fursa ya ufikiaji wa masoko na wajasiriamali kupata washauri wengi wenye uzoefu tofauti hasa kwenye upatikanaji wa mitaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa AUDA-NEPAD, Ibrahim Assane Mayaki amesema wakati bara la Afrika linakabiliwa na hali ya kutokuwa na uhakika wya kiuchumi na kijamii kutokana na mlipuko wa COVID-19, Taasisi ya AUDA-NEPAD, inakusudia kukuzauwezo wa kujikinga na athari zinazojitokeza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |