Benki kuu ya Uganda imesema iytaendelea kudumisha viwango vya riba kwa asilimia 7 lakini ikaonya kuwa mfumuko wa bei unaweza kuongezeka zaidi hadi asilimia 6.1 katika robo ya kwanza ya 2021.
Akiwasilisha sera ya kifedha ya mwezi Agosti, gavana wa Benki ya kuu hiyo Emmanuel Tumusiime Mutebile alisema dhamira ya Kamati ya Sera ya Fedha ni kufikia Kiwango cha Bei ya Watumiaji (CPI) cha asilimia 5 .
Mfumko mkubwa wa bei huathiri uwezo wa kununua kutokana na kupanda kwa bei za bidhaa na huduma katika uchumi zinazohitaji watu kuwa na pesa zaid.
Pia huongeza gharama ya kukopa pesa kutoka benki na kampuni na watu binafsi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |