Benki Kuu ya Rwanda imedumisha kiwango cha uwekezaji kwa asilimia 4.5 kwa benki za kibiashara ili kuhimiza benki hizo kutoa mikopo kwa watu na sekta binafsi .
Hii inafuatia mkutano wa Kamati ya Sera ya Fedha uliofanywa jana ili kupitia maendeleo ya hivi punde ya kiuchumi duniani na kitaifa pamoja na uwezo wa kuingilia kati.
Benki Kuu ya Rwanda mwezi Aprili ilishusha kiwango chake cha uwekezaji kwa benki za kibiashara kutoka asilimia 5 hadi asilimia 4.5 ikiwa na lengo la kuongeza utoaji mikopo kwa sekta binafsi ili kusaidia ufufuaji wa uchumi kufuatia janga la Corona.
Kwa kushukisha kiwango hicho,inafanya benki kuzingatia kutoa mikopo ,jambo ambalo litasukuma ufufuaji wa uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |