• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Serikali yaagiza halmashauri zote kuanza maandalizi ya ujenzi wa miradi

    (GMT+08:00) 2020-08-19 17:09:25

    Serikali ya Tanzania imeziagiza halmashauri zote nchini, kuanza maandalizi ya ujenzi wa miradi ya maendeleo inapoainishwa ili kurahisisha utekelezaji wake fedha zinapotolewa na Serikali.

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Joseph Nyamhanga, ndiye aliyetoa agizo hilo juzi akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Jiji la Dar es Salaam.

    Alisema amekutana na changamoto za fedha kusubiri maandalizi ya utekelezaji wa miradi, badala ya utekelezaji kusubiri fedha, hali inayozidi kuchelewesha miradi ya maendeleo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako