• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • CAF yatangaza ratiba ya michezo ya kufuzu Kombe la Afrika na Kombe la dunia

    (GMT+08:00) 2020-08-21 17:43:25

    Shirikisho la soka Afrika (CAF) limetangaza rasmi ratiba ya mashindano ya kuwania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) na Kombe la Dunia, ambayo yanarejea baada ya kusimama kwa muda mrefu kutokana na tatizo la virusi vya Corona. Ratiba iliyotolewa juzi na Caf, imeonyesha kuwa mechi za kuwania kufuzu fainali za Afcon mwaka 2021 zitakazofanyika Cameroon na zile za Kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar mwaka 2022 zitachezwa kuanzia Novemba 9 mwaka huu na zitahitimishwa rasmi Novemba 16 mwaka huu. Baada ya kuchezwa kwa raundi mbili ambazo ni ya kwanza na ya pili, mechi za raundi ya nne na ile ya tano ya mashindano ya kuwania kufuzu Afcon 2021, zimepangwa kuchezwa kati ya Novemba 9 hadi 15 mwaka huu kwa mujibu wa ratiba hiyo iliyotolewa na Caf.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako