Kusaya aliwataka Watanzania kuanzisha viwanda vya mbolea ambayo inahitajika kwa wingi zaidi wakati huu kilimo kikiwa ni biashara na kinaajiRi asilimia 58 wananchi na kuchangia malighafi za viwandani kwa asilimia 65.
Alisema mahitaji ya mbolea za viwandani yameongezeka nchini kutokana na hamasa kubwa na wakulima kujitokeza kulima zaidi ikiwa ni mafanikio yaliyopatikana na Wizara ya Kilimo kwa ushirikiano na sekta binafsi.
Alisema mahitaji ya mbolea kwa mwaka ni tani 664,000 wakati uzalishaji kwenye viwanda umefika tani 30,000 ya mbolea hivyo kuwa na uhitaji mkubwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |