• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • TADB yatoa milioni 450 kwa kiwanda Cha nyama Tanzania

    (GMT+08:00) 2020-08-28 18:44:22
    Waziri wa Mifugo na Uvuvi nchini Tanzania Luhaga Mpina ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini humo (TADB) kwa kutoa mkopo wa masharti nafuu wa shilingi milioni 450 kwa kiwanda cha nyama nchini humo .

    Waziri Mpina, alieleza kufurahishwa na mkakati wa TADB wa kuinua sekta muhimu za uchumi na kuziomba benki nyingine kuunga mkono azma ya serikali ya ujenzi wa uchumi wa viwanda

    TADB imekipa kiwanda cha Meat King Distributors fedha kuboresha miundombinu ili kuongeza uzalishaji na kwa kununua ng'ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe za wafugaji. Waziri Mpina amesifu juhudi hiyo ya TADB.

    Mpina alisema wizara yake itaendelea kuunga mkono wawekazaji katika viwanda ambavyo malighafi zake zinategemea mifugo na kusema wizara yake itahimiza ufugaji wa kisasa utakaomfanya mfugaji anufaike zaidi na mifugo yake.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako