Chama cha Wafanyabiashara wa Miraa cha Nyambene (Nyamita) kimesema kuwa mazungumzo ya kumaliza mzozo wa biashara hiyo yamegonga mwamba na Somalia imetoa masharti ambayo lazima yashughulikiwe na Kenya.
Masharti hayo ni pamoja na; Kenya lazima iichukue Somalia kama mshirika mwenza, kuepuka kuingilia mambo ya ndani ya Somalia, iombe radhi kwa kukiuka amri za anga ya Somalia, iruhusu bidhaa kutoka Somalia ikiwa ni pamoja na samaki, mchele, sukari, asali, nyama na maziwa na Kenya kuacha kulazimisha safari kutoka Somalia kutua kwanza mjini Wajir kwa ukaguzi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |