Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Mabula Mchembe, alisema hayo jana wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya Siku ya Tiba Asilia ya Mwafrika katika viwanja vya Nyerere Square, jijini Dar es Salaam.
Alisema, waganga wa tiba asili wanatakiwa kuitumia fursa hiyo kwa kuanzisha viwanda vidogo vitakavyokuwa na uwezo wa kuchakata dawa zenye viwango.
Prof. Mchembe alisema kwa kutumia viwanda vidogo, waganga hao watazalisha dawa nyingi na zenye viwango ili kuziuza ndani na nje ya nchi,na kujikwamua kiuchumi na kuongeza pato la taifa.
Aliliagiza Baraza la Taifa la Tiba Asili na Tiba Mbadala kuongeza jitihada katika kusajili dawa zinazotengezwa na waganga nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |