• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • WAFUGAJI WAONYWA KUHUSU UWEZEKANO WA UKAME KENYA.

    (GMT+08:00) 2020-09-04 16:42:56
    Idara ya Utabiri wa Hewa nchini Kenya imewaonya wakazi wa maeneo ya kaskazini na kusini mwa nchi kuhusu uwezekano wa kupoteza mifugo wao kutokana na kupungua kwa malisho.

    Kwenye utabiri wake kuhusu hali ya hewa mwezi huu, idara ilionya kwamba maeneo hayo yataendelea kushuhudia hali kame.

    Ilieleza kwamba maeneo ya Marsabit, Isiolo, Wajir, Mandera na Garissa katika eneo la kaskazini yatakumbwa na hali hiyo, sawa na maeneo ya Machakos, Makueni, Kituo na Taita Taveta.Maeneo mengine yatakayoshuhudia hali kame ni Kajiado na Narok.

    Hivyo, wenyeji wameshauriwa kujitayarisha mapema, ili kuepuka hali ambapo mifugo wao watafariki kutokana na ukosefu wa malisho ya kutosha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako