Kwenye utabiri wake kuhusu hali ya hewa mwezi huu, idara ilionya kwamba maeneo hayo yataendelea kushuhudia hali kame.
Ilieleza kwamba maeneo ya Marsabit, Isiolo, Wajir, Mandera na Garissa katika eneo la kaskazini yatakumbwa na hali hiyo, sawa na maeneo ya Machakos, Makueni, Kituo na Taita Taveta.Maeneo mengine yatakayoshuhudia hali kame ni Kajiado na Narok.
Hivyo, wenyeji wameshauriwa kujitayarisha mapema, ili kuepuka hali ambapo mifugo wao watafariki kutokana na ukosefu wa malisho ya kutosha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |