• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • TANZANIA: SERIKALI YAPOKEA GAWIO LA BILIONI 33 KUTOKA KWA AIRTE

    (GMT+08:00) 2020-09-04 16:43:36
    Serikali kuu imepokea kiasi cha shilingi bilioni 33.99, likiwa ni gawio na mchango kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania. Makabidhio hayo, yalmefanyika jijini Dodoma, ambapo katibu mkuu wa Wizara ya Fedha ma mipando, Dotto James, alipokea kwa niaba ya serikali.

    Akizungumza wakati wa kukabidhi hundi, mwenyekiti wa bodi ya Airetl Tanzania, Pascal Malata, alisema kiasi hicho cha fedha ni sehemu ya faida iliyopata kampuni.

    Malata alisema shilingi bilioni 18.99 zimetolewa kama gawio serikalini kutokana na kuwa na hisa za asilimia 49, Airtel ikibaki kumiliki hisa za asilimia 51 kwenye kampuni. Alisema pia Airtel imetoa shilingi bilioni 14 ukiwa mchango wa kampuni kwa jamii katika maeneo ya kutoa huduma mbalimbali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako