Baraza la Afya yaUmma la Maonesho ya kimataifa ya biashara ya hudumua ya China mwaka 2020 limefanyika jana, ambapo limetoa "Mwito wa Beijing", likizitaka pande mbalimbali kukusanya busara za dunia kupambana na COVID-19, kupambana kwa pamoja na matishio ya magonjwa duniani, kujenga uhusiano wa wenzi wa ushirikiano wa karibu zaidi, kufungua na kufanya ushirikiano, na kuhimiza usalama wa afya ya umma duniani.
Mwito huo umesema, nchi yoyote haiwezi kuwa peke yake wakati binadamu wanapokabiliwa na matishio makubwa ya afya, na ushirikiano wa afya wa kimataifa unaweza kuonesha umuhimu mkubwa katika kulinda utaratibu wa dunia na kuhimiza maendeleo ya uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |