Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Zhao Lijian amesema, hivi sasa dunia bado inakabiliwa na janga la COVID-19, na China inapenda kuendelea kusukuma mbele ushirikiano wa kimataifa, ili kulishinda janga hilo.
Bw. Zhao amesema China itaendelea kuliunga mkono Shirika la Afya Duniani kufanya kazi ya uongozi katika juhudi za kimataifa za kukabiliana na virusi vya Corona, kubadilishana uzoefu wa kukinga kutibu virusi vya Corona na nchi nyingine, na kuendelea kutoa msaada kwa nchi zisizo na uwezo wa kutosha wa kupambana na virusi hivyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |