• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mafuriko yaathiri biashara jijini Kampala

    (GMT+08:00) 2020-09-10 18:33:54

    Wafnyabiashara katika jumba la biashara la Mutaasa-Kafeero katika barabara ya Luwum jijini Kampala ,jana walipoteza bidhaa zao,kufuatia mafuriko ambayo yaliziba maduka yao baada ya mvua kubwa kunya majira ya asubuhi.

    Musa Kawesa ,mfanyabiashara wa simu na bidhaa za simu alisema alipata hasara ya zaidi ya Sh15mn.

    Mitaa na barabara nyingi jijini Kampala zilikuwa hazipitiki na madereva wengi walipata tabu kuendesha magari katika mafuriko hayo.

    Wasafiri katika barabara ya Mukwano,Sixth Street katika eneo la Viwandani na barabara ya Jinja pia walipata hasara baada ya pikipiki na mali zao kutekwa na mafuriko.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako