Waziri mkuu wa serikali ya maafikiano ya kitaifa ya Libya Bw. Fayez al-Sarraj amesema atakabidhi madaraka kwa mrithi wake kabla ya mwisho wa mwezi Oktoba.
Bw. al-Sarraj amesema hayo alipohutubia taifa Jumatano kwa njia ya televisheni ya taifa. Ametoa wito kwa Tume ya Mazungumzo kuunda taasisi mpya za utawala, ili kuhakikisha makabidhiano ya madaraka yanafanyika kwa amani na utulivu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |