• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: KQ yaanza safari zake kwenda Tanzania

    (GMT+08:00) 2020-09-22 19:20:51

    Kenya Airways imeanza tena safari za ndege kwenda Tanzania kufuatia kuondolewa kwa kusimamishwa kwa waendeshaji wote wa anga wa Kenya na Serikali ya Tanzania.

    Hii inafuatia duru iliyotolewa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania ikitangaza kufungua tena na kurejesha ndege zote na waendeshaji wa Kenya mara moja.

    Ndege ya kwanza ya Kenya Airways kwenda Dar es Salaam iliondoka Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta - Nairobi mwanzoni mwa wiki na ya pili jioni ya Jumatano tarehe 23 Septemba.

    Kwa hiyo KQ itafanya safari mbili za kila siku kwenda Dar es Salaam.

    Ndege ya kwanza ya KQ kwenda Zanzibar itaondoka Jumamosi tarehe 26 Septemba na baadaye itafanya kazi mara tatu kwa wiki - Jumatatu, Jumatano na Jumamosi.

    Ndege za kwenda uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro zitaanza tena Oktoba.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako