Mkutano wa Umoja wa Ulaya waahirishwa kutokana na rais wa baraza la Umoja huo kuwekwa karantini
Rais wa Baraza la Ulaya Charles Michel ameahirisha Mkutano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya baada ya kuwekwa karantini Jumanne.
Rais huyo aligundua kuwa, ofisa usalama ambaye aliwasiliana naye kwa karibu wiki iliyopita, alikutwa na virusi vya Corona. Ingawa rais huyo jana alipimwa na kukutwa hana maambukizi, aliamua kujiweka karantini kwa mujibu wa kanuni za Ubelgiji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |