Takwimu zilizotolewa Jumanne na serikali ya Uingereza zimeonyesha kuwa, watu 4,926 wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona nchini humo, ikiwa ni ongezeko kubwa zaidi kwa siku tangu tarehe 7 mwezi Mei.
Takwimu hizo zimeonesha kuwa, idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona nchini Uingereza imefikia 403,551, na idadi ya vifo vinavyotokana na virusi hivyo imefikia 41,825.
Mapema Jumanne, waziri mkuu wa Uingereza Bw. Boris Johnson alitangaza hatua mpya za vizuizi ili kukabiliana na kuongezeka kwa kasi kwa maambukizi ya COVID-19 nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |