• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RWANDA: KAMPUNI ZA MADINI ZAPATA MWELEKEO MPYA.

    (GMT+08:00) 2020-09-25 16:16:25

    MTENDAJI Mkuu wa Bodi ya Migodi ya Rwanda, Petroli na Gesi (RMB) Francis Gatare,amesema kuna matumaini kwamba sekta ya madini nchini humo hivi karibuni itapona kutokana na athari mbaya zilizotokana na janga la Covid-19.

    Sekta ya madini ya Rwanda, kama sekta nyengine ulimwenguni, imeathiriwa vibaya na janga hilo, haswa kwa sababu ya kufungiwa na serikali kusitisha shughuli zote.

    Sekta hiyo imeathiriwa sana na kushuka kwa bei za kimataifa za madini kutokana na nguvu ndogo ya ununuzi kama matokeo ya janga hilo.

    Vizuizi vya nchi tofauti juu ya safari za anga pia vilifanya iwe vigumu kusambaza madini.

    Kitakwimu, mauzo ya mapato ya nchi ya 3Ts yalipungua kwa asilimia 30.9 kwa sababu ya kushuka kwa bei za bidhaa za kimataifa mnamo Januari na Februari 2020 ikilinganishwa na kipindi kama hicho cha 2019.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako