Rais wa Marekani Donald Trump mapema leo ametangaza kuwa yeye na mke wake mama Melania wamegundulika kuambukizwa COVID-19, baada ya mhudumu wao kupata virusi vya ugonjwa huo.
Kwenye mtandao wa Tweeter Trump amesema wataanza kujitenga na mchakato wa kupona mara moja. Tangazo hilo limekuja saa kadhaa baada ya Trump kuthibitisha kwamba mshauri wa Ikulu ya White House Hope Hicks amepata virusi vya Corona.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |