• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jamii ya kimataifa yatarajia kuimarisha ushirikiano na China katika kukabiliana na virusi vya Corona

    (GMT+08:00) 2020-10-05 16:56:44

    Nchi mbalimbali zimeeleza nia ya kuimarisha ushirikiano na China katika juhudi za kukabiliana na virusi vya Corona.

    Waziri wa habari wa Zimbabwe Monica Mutsvangwa ameishukuru China kwa kuipatia Zimbabwe misaada ya vifaa vya kinga na matibabu, na kusema China ilipeleka wataalamu wa kiafya nchini Zimbabwe, ambao walitoa uzoefu muhimu kuhusu jinsi ya kukinga na kutibu virusi vya Corona.

    Hadi sasa kutokana na ushirikiano wa China na Afrika, vifaa vya kukabiliana na virusi vya Corona vimepelekwa hadi nchi 20 za Afrika ambazo hazina bandari, na China imepeleka timu za wataalamu wa afya kwenda nchi 13 barani Afrika. Mkurugenzi wa mambo ya kisiasa wa chama tawala cha Kenya Jubilee Kadara Swaleh amesema, China imetoa misaada mingi ikiwemo teknolojia, uzoefu na vifaa kwa sehemu mbalimbali duniani. Katika msukosuko huo, China inajitahidi kuziunganisha nchi mbalimbali na kutoa mchango wake, badala ya kuifarakanisha dunia. Amesisitiza kuwa, ni wakati kwa binadamu kukaa pamoja kujadili ufumbuzi wa masuala yakiwemo chanjo na ukarabati wa uchumi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako