Chumba cha mkutano cha Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kimeanza kutumika tena baada ya kufungwa kwa miezi 7 kutokana na janga la COVID-19, ambapo jana Baraza hilo lilifanya mkutano wa hadhara kujadili hali ya Mali. Ikiwa ni hatua za kukabiliana na virusi vya Corona, vioo viliweka kati ya viti, waliohudhuria mkutano walipungua na wote walivaa barakoa na kukaa kwa umbali. Kutokana na athari za virusi vya Corona, baraza hilo lilikuwa likifanya mkutano kwa njia ya video kuanzia katikati ya mwezi Machi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |