Mke wa rais wa China ambaye pia ni mjumbe maalumu wa kuhimiza elimu ya watoto wa kike na wanawake kwenye Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO, Bibi Peng Liyuan, ametoa salamu za pongezi kwa njia ya video kwenye tuzo ya elimu ya UNESCO kwa watoto wa kike na wanawake. Bibi peng amewapongeza watu waliopewa tuzo hiyo kutoka Sri Lanka na Kenya, na kusema China itaendelea kuhimiza mawasiliano na ushirikiano wa elimu ya kimataifa, kutoa mchango mkubwa zaidi kwa ajili ya kuhimiza elimu ya watoto wa kike na wanawake, na kutimiza malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ya kuelekea mwaka 2030. Katibu mkuu wa UNESCO Bibi Audrey Azoulay amesifu na kuishukuru serikali ya China kwa kuunga mkono tuzo hiyo, na kusisitiza kuwa shirika hilo linapenda kushirikiana na pande mbalimbali, kuhimiza watoto wa kike na wanawake duniani kupata fursa sawa za elimu na mustakabali mzuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |