• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Chuo kikuu cha Tsinghua cha China chatafuta ushirikiano wa kitaaluma na vyuo vikuu vya Afrika

    (GMT+08:00) 2020-10-14 08:38:40

    Chuo kikuu cha Tsinghua, ambacho ni moja ya vyuo vikuu maarufu zaidi nchini China, kinatafuta ushirikiano wa kitaaluma na vyuo vikuu vya Afrika, ili kusaidia kuandaa raslimali watu kwa ajili ya maendeleo ya bara hilo.

    Naibu mkuu wa Chuo kikuu cha Tsinghua Yang Bin alisema hayo kwenye mkutano uliofanyika kwa njia ya video na Chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Kwame Nkrumah cha Ghana, ikiwa ni sehemu ya programu ya wiki ya uchumi na utamaduni kati ya Ghana na China. Yang amesema chuo kikuu cha Tsinghua kinatafuta kujenga muundo wa elimu ulio shirikishi na wenye ustahimilivu na washirika wake wa Afrika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako