• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda yaanza kutoa huduma ya kingamwili kwa waliokosa kutokana na zuio la COVID-19

    (GMT+08:00) 2020-10-14 18:43:57

    Uganda imeanza kutoa huduma ya kingamwili kwa watoto na watu wazima zaidi ya milioni 38.4 ambao walikosa huduma za chanjo ya lazima kutokana na zuio la COVID-19.

    Msemaji wa Wizara ya Elimu Emmanuel Ainebyoona amesema wizara yake inaendesha kampeni ya chanjo ya Oktoba, inayoitwa Siku za Kukamilisha Afya ya Mtoto, ili kupunguza magonjwa yanayozuilika, vifo na ulemavu yanayotokana na kuharisha, nimonia, surua, tetenasi, kifua kikuu na saratani ya kizazi, miongoni mwa mengine.

    Bw. Ainebyoona amesema jumla ya watoto wa kike milioni 1.2 wenye umri kati ya miaka 10 na 11 wanapatiwa kinga ya saratani ya kizazi, watoto milioni 17.3 wenye umri chini ya miaka 15 wanapewa tiba ya kuondoa minyoo, na watoto milioni 7.5 wenye umri chini ya miaka mitano wanapaswa kupokea dawa za Vitamin A ili kuwalinda na upofu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako