Awamu ya tatu ya maonyesho ya kimataifa ya uagizaji bidhaa wa China itafanyika mwezi ujao mjini Shanghai. Msemaji wa Wizara ya biashara ya China Bw. Gao Feng amesema kuwa, ukubwa wa eneo la biashara katika maonyesho ya mwaka huu umeongezeka kuliko mwaka jana, na kazi mbalimbali zinaendelezwa kwa utaratibu.
Bw. Gao Feng amesema, eneo la biashara litakuwa na sehemu sita, zikiwemo chakula na bidhaa za kilimo, magari, vifaa vya tenkonojia, bidhaa za matumizi, vifaa vya matibabu na dawa, na biashara ya huduma.
Ameongeza kuwa, chini ya hali ya kawaida ya kinga na udhibiti wa maambukizi ya virusi vya Corona, maonyesho ya mwaka huu yanatoa kipaumbele kwenye usalama na kuimarisha hatua za kinga na udhibiti wa virusi vya Corona. Hivi sasa kazi ya maandalizi ya maonyesho hayo inaendelezwa kwa utaratibu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |