Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Mali (MINUSMA) imethibitisha kuwa askari mmoja wa kulinda amani wa tume hiyo aliuawa na mwengine kujeruhiwa vibaya baada ya gari lao kukanyaga bomu la kutegwa ardhini jana alasiri kilomita 50 kutoka mji wa Kidal, kaskazini mashariki mwa Mali. Tume hiyo imelaani vikali mashambulizi hayo holela dhidi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, vikosi vya Mali na vya kimataifa na hata raia wasio na hatia, na pia imesisitiza kuwa mashambulizi hayo yanachukuliwa kama uhalifu wa kivita kwa mujibu wa sheria ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |