Guinea jana ilifanya uchaguzi wa urais, wagombea 12 wameshiriki kugombea urais kwenye uchaguzi huo akiwemo rais wa sasa Bw. Alpha Condé.
Takwimu kutoka tume ya uchaguzi ya taifa ya Guinea inasema idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura ilizidi milioni 5. Vyombo vya habari vya nchi hiyo vinaona kuwa uwezekano wa Bw. Conde kushinda tena ni mkubwa, kutokana na kuwa na wafuasi wengi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |