Serikali ya Sudan na ICC hawajafikia makubaliano juu ya utaratibu wa kuwahukumu washukiwa wanaotafutwa
Waziri wa Sheria wa Sudan Nasr-Eddin Abdul-Bari amesema serikali ya Sudan na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC bado hazijakubaliana juu ya utaratibu maalumu wa kuwahukumu washitakiwa wanaotafutwa kwenye sehemu ya Darfur.
Bw. Abdul-Bari amesema Sudan imewasilisha mapendekezo matatu kwa ICC nayo ni pamoja na kuanzisha mahakama ya pamoja, washitakiwa wahukumiwe kwenye ICC, au kuanzisha mahakama maalumu nchini Sudan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |