• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri mkuu wa Somalia atangaza baraza jipya la mawaziri

    (GMT+08:00) 2020-10-20 21:04:15

    Waziri mkuu wa Somalia Bw. Mohamed Hussein Roble ametangaza rasmi baraza la mawaziri, linalotarajiwa kuongoza nchi wakati wa uchaguzi ujao.

    Kwenye taarifa aliyotoa jana jioni, Bw. Roble amewateua mawaziri 27, mawaziri wa nchi 17 na manaibu waziri 26. Amesema kwenye uundaji wa baraza hilo amepata maoni ya wasomi na watu mbalimbali katika jamii, na kutoa kipaumbele kwa vijana na wanawake kwenye nafasi muhimu. Baraza hilo lenye mawaziri wanne wanawake, linatakiwa kuidhinishwa na bunge kabla ya kuanza kutekeleza majukumu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako