Jeshi la Iraq limegundua kaburi moja lenye maiti za watu zaidi ya 50 wanaoaminika kuuawa na kundi la IS jimboni Kirkuk.
Msemaji wa kamanda mkuu wa jeshi Bw. Yehia Rasool amesema, polisi wamegundua kaburi hilo wakati walipokuwa wakiwasaka wapiganaji wa kundi la IS.
Habari zinasema, wapiganaji wa kundi la IS wameongeza mashambulizi dhidi ya vikosi vya usalama na raia katika jimbo walilolidhibiti zamani la Sunni na kusababisha vifo na majeruhi ya watu wengi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |