Waziri mkuu wa Tanzania Bw. Kassim Majaliwa amesema, Tanzania inapanga kujenga reli mpya yenye umbali wa kilomita 1,000 kusini mwa nchi hiyo.
Taarifa iliyotolewa jana na ofisi ya waziri mkuu imesema, uchunguzi wa uwezekano na miundo wa usanifu kuhusu ujenzi wa reli hiyo imekamilika.
Akiongea kwenye mkutano wa hadhara mkoani Mtwara siku ya Jumanne Bw. Majaliwa alisema, ujenzi wa reli hiyo kutoka bandari ya Mtwara hadi Mchuchuma na Liganga yanapopatikana madini ya chuma na makaa ya mawe utakuwa sehemu moja ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama tawala cha Mapinduzi ya mwaka 2020 hadi 2025.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |