Ripoti ya Makadirio ya Ukuaji wa Uchumi kwenye sehemu ya Asia na Pasifiki iliyotolewa na Mfuko wa Fedha wa Kimataifa IMF imesema, uchumi wa sehemu hiyo umeanza kufufuka kutoka hali ya kupungua iliyotokana na janga la COVID-19, lakini kasi za makundi tofauti ya kiuchumi ni tofauti.
Ripoti hiyo imesema kutokana na kufufuka kwa nguvu kwa uchumi katika robo ya pili mwaka huu, ongezeko la uchumi wa China linatazamiwa kufikia asilimia 1.9, na China litakuwa kundi pekee la kiuchumi litakalotimiza ongezeko la uchumi kati ya makundi makubwa ya kiuchumi duniani mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |