Mfanyakazi wa zamani wa Shirika la Usalama la Kitaifa la Marekani Edward Snowden amepata kibali cha ukaazi wa kudumu nchini Urusi.
Mwaka 2013 Snowden alifichua kuwa mashirika ya ujasusi ya Marekani yanawachunguza watu wengi kupitia mipango kama PRISM, yakiwalenga hata viongozi wa nchi na serikali ambao ni wenzi wa Marekani. Baada ya hapo alikimbilia Urusi na kusakwa na Marekani kwa tuhuma za kufanya mambo ya ujasusi na kuiba mali za serikali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |