Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Shelisheli Bw. Danny Lucas jana Jumapili alitangaza kuwa mgombea urais wa upinzani Bw. Wavel Ramkalawan kutoka chama cha Seychelles Democratic Union amepata ushindi kwenye uchaguzi wa urais kwa kupata asilimia 54.9 ya kura.
Rais Danny Faure ambaye pia ni mgombea kutoka chama cha United Seychelles amepata asilimia 43.5 ya kura. Bw. Wavel Ramkalawan mwenye umri wa miaka 59 alishindwa mara tano kwenye uchaguzi wa urais, na sasa aligombea kwa mara ya sita kwake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |