Msemaji wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema mashirika ya kibinadamu yanasaidia kutoa msaada wa chakula kwa wakimbizi wa ndani zaidi ya elfu kumi waliokimbia machafuko kaskazini mwa Msumbiji katika siku kumi zilizopita.
Msemaji huyo amesema Umoja wa Mataifa na washirika wake wametoa chakula na maji kwa zaidi ya watu elfu tano, na kwamba zaidi ya watu laki tatu wamekimbia makazi yao na wanahitaji msaada wa kuokoa maisha kutokana na machafuko yanayoendelea kwa miezi kumi iliyopita mkoani Cabo Delgado.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |