Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limehimiza pande kinzani nchini Libya kutimiza ahadi yao na kutekeleza kikamilifu makubaliano yaliyofikiwa.
Taarifa iliyotolewa wa Baraza la Usalama inasema, wajumbe wa baraza hilo wanakaribisha makubaliano ya usitishaji vita wa kudumu yaliyosainiwa na Tume ya Pamoja ya Kijeshi ya 5+5 huko Geneva kufuatia mazungumzo yaliyodhaminiwa na Umoja wa Mataifa, na wajumbe hao pia wametoa wito kwa pande kinzani nchini Libya kuonesha dhamira ya kufikia suluhu ya kisiasa kupitia Jukwaa la Mazungumzo ya Kisiasa la Libya (LPDF).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |