Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema, mikutano ya ana kwa ana iliyopangwa kufanyika jana imefutwa baada ya wanadiplomasia watano wa ujumbe wa kudumu kwenye Umoja wa Mataifa kukutwa na virusi vya Corona.
Bw. Dujarric amesema, idara ya matibabu ya Umoja wa Mataifa ilianza mara moja mchakato wa kufuatilia watu waliokuwa karibu na wanadiplomasia hao.
Kufuatia hali hiyo, mikutano ya ana kwa ana iliyokuwa ifanyike leo imefutwa, na hali hiyo inakadiriwa kuendelea kwa siku kadhaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |