Waziri wa mahusiano na ushirikiano wa kimataifa wa Afrika Kusini Bi. Naledi Pandor amesema wenzake kutoka Ethiopia, Misri na Sudan watakutana tena ndani ya siku saba kujadili suala la Bwawa la GERD la Ethiopia.
Bi. Pandor ametoa kauli hiyo baada ya mkutano uliofanyika Jumanne kwa njia ya video kati yake na mawaziri wa maji wa Ethiopia, Misri na Sudan. Amesema pande zote husika zimerejea ahadi zao kwa mazungumzo yatakayofanyika wiki hii baada ya kushindwa kufikia mwafaka miezi miwili iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |