Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu, OCHA limesema watu wasiopungua 35 wamefariki dunia na wengine wapatao milioni 1.6 wameathiriwa kutokana na mafuriko nchini Somalia tangu mvua kubwa zianze kunyesha mwezi Januari.
Kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa na OCHA, watu laki 7.16 wamepoteza makazi yao na mashamba na miundombinu vimeharibika, hali inayoongeza hatari ya kuenea kwa magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya maji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |