Kutokana na kukaribia kwa Maonesho ya tatu ya bidhaa za kimataifa ya China CIIE, wafanyabiashara wengi wa Zambia wameeleza matarajio yao kuwa maonesho hayo yatahimiza biashara zao.
Walipohojiwa na shirika la habari la China Xinhua, wafanyabiashara hao wameeleza matumaini kuwa maonesho hayo si kama tu yanaweza kufufua biashara, bali pia yatasaidia kuanzisha mchakato wa kufufuka kwa uchumi wa dunia.
Mfanyabiashara wa asali Bibi Clementine Mwaba amesema mazao mengi ya kilimo ya Zambia yanahitaji masoko zaidi ya kimataifa, na maonesho ya CIIE yatatoa fursa ya kuingia kwenye soko la bidhaa hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |