Taarifa ya kikao cha Mkutano wa 5 wa awamu ya 19 ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) uliofanyika kuanzia tarehe 26 hadi tarehe 29 Oktoba imetolewa leo hapa Beijing.
Katibu mkuu wa Kamati hiyo Xi Jinping amehutubia mkutano huo.
Kikao hicho kimesikiliza na kujadili ripoti ya kazi ambayo rais Xi amewasilisha kwa niaba ya ofisi ya siasa ya Kamati Kuu ya CPC.
Kikao hicho pia kimepitisha mapendekezo ya Kamati Kuu ya CPC ya kutunga Mpango wa 14 wa Maendeleo ya Uchumi na Jamii wa Miaka Mitano (2021-2025) na malengo ya muda mrefu ya kufikia mwaka 2035.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |