Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Msumbiji hivi karibuni vimewaua magaidi 108 kwenye operesheni ya kupambana na ugaidi inayoendelea mkoani Cape Delgado, kaskazini mwa nchi hiyo.
Akihutubia bunge la nchi hiyo waziri mkuu wa Msumbiji Bw. Carlos Agostinho do Rosario amesema shughuli za kigaidi kwenye sehemu ya kaskazini ya nchi hiyo zimesababisha watu zaidi ya laki nne kukimbia makazi yao, na serikali inawasaidia kurudi kwenye maisha ya kawaida. Wakati huohuo, serikali pia itaongeza uwezo wa kupambana na ugaidi na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa kwenye nyanja hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |