Jumla ya wanamgambo 22 wa kundi la Boko Haram waliuawa na vikosi vya Nigeria kwenye operesheni iliyofanyika hivi karibuni ya kuwasaka wapiganaji waliobaki wa kundi hilo kwenye sehemu ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Msemaji wa Jeshi la Nigeria Bw. Benard Onyeuko amesema operesheni iliyofanyika Oktoba 25 katika mji wa Damboa, kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno, ilikuja kufuatia jaribio la magaidi kuvamia kituo kimoja cha jeshi kwenye eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |